Slaus Technologies Tz1
 

Harakati za jiji Harakati za jiji Author
Title: PAUL MAKONDA AFANYA TUKIO HILI LA MFANO MKOA WA DAR ES SALAAM
Author: Harakati za jiji
Rating 5 of 5 Des:
Na Frank Wandiba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amewataka wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kutunza mazingira hasa sehemu ...

Na Frank Wandiba
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amewataka wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kutunza mazingira hasa sehemu zenye mazalia ya mbu ili kuepukana na ugonjwa wa mabusha na matende.Makonda ametoa wito huo siku ya leo.

Akizungumza na wananchi wa  Kata ya Buguruni  wakati akizindua kampeni ya uhamasishaji unywaji dawa na kufanyiwa upasuaji kwa magonjwa yasiyopewa kipaumbele ambayo ni Matende, Mabusha, Kichocho, Minyoo na Usubi, ambapo kwa mujibu wa takwimu zinaonesha wakazi wa Dar es Salaam wamekuwa wakisumbuliwa na magonjwa hayo hasa minyoo, matende na mabusha.

Mhe Makonda alisema ni vyema wakazi wa Dar es Salaam wakaitumia fursa hiyo ya kampeni itakayodumu kwa siku tano kuanzia mpaka Oktoba 30, kwa kujitokeza kwa wingi kupimwa na kunywa dawa kutaisaidia serikali kuinua nguvu kazi hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi kwani watu wakiugua maradhi hayo bila ya kupata tiba au kuwa na kinga mapema hupoteza nguvu kazi.

Mhe Makonda aliongeza kuwa takribani ya watu 6400 wamegundulika na mabusha hivyo ni vyema wakawahi mapema kupatiwa matibabu pamoja na kutoa wito kwa wenanchi wa mkoa wa dar na maeneo ya jiarani wajitokeze kwa wingi hili kuweza kupita lengo la idadi ya wananchi milioni 3.9 waliojitokeza wakati wa zoezi hilo mwaka 2009.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dokta Grace Maghembe amewataka wakazi hao kutosikiliza upotoshaji wa kuwa wakitumia dawa hizo hawatakuwa na uwezo wa kupata watoto na badala yake wajitokeze kwa wingi kwani dawa hizo ni salama, huku akisisitiza kuwa kwa zoezi la unywaji wa dawa litafikia tamati Oktoba 30, wakati zoezi la upasuaji litakuwa  likiendelea mpaka mwezi Desemba.

Bi Maghembe Alisema zoezi la upasuaji kwa watu wenye mabusha linaloendelea kituo kilichopo Pugu zaidi ya watu 76 wameshapatiwa  matibabu aidha amelibainisha katika kuhalikisha wanasogeza huduma hiyo karibu zaidi kwa wananchi wamejipanga kuongeza vituo vingine kuendesha zoezi hilo katika maeneo mengine ya jiji la dar.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top